kwale

kwale

Translate; UNAWEZA KUITAFSIRI BLOG HII KWA LUGHA ZAIDI YA 60

ELIMU MAALUM JUU YA UFUGAJI NA UTUNZAJI WA KWALE

The Japanese Quail (Coturnix Japonica) originates from Eastern Asia. In a wild quails are migratory birds living in grassland and cultivated fields. The colour of the Japanese quail is typically speckled

A pair of Japanese Quail sitting in the grassyellow-brown, with a light creamy strip running from the eyes towards the back of the head, but quail can also come in other colours like white, white-black, speckled red-brown or cream-brown. An adult quail will reach around 20cm (7 ¾ Inch) in height and around 150g (5 ounces) in weight. Their domestication has began as early as in the fourteen century. At first quails became popular as game birds but at later stage the commercial keeping of quail has kicked off because of their tasty eggs and meat. The biggest commercial revolution of the quail began after 1910 when they were divided into two groups; for egg production and for the table. Nowadays the quail is not the most popular little bird among bird keepers even though it would deserve a lot more attention. Quail can be kept in cages or small aviary enclosures covered with tightly woven mesh. On a small scale you can keep 10 to 15 quails in 1 square meter floor area. This amount of quail will provide enough eggs for a family of four. The keeping of quail on a small scale is fairly simple. Quails like to stay on the floor, hardly ever jump up onto higher places, which means that if you’ve had an aviary already in place with other birds in it, you could just place some quail in there and they would be happy to pick up every edible particle from the floor that the other birds may drop. If kept outside, you would have to provide a draught free zone (shelter) for the quail where they can hide from the bad weather. In outside conditions the quail will stop laying eggs during the colder winter period but if kept inside under good conditions like enough space, food, temperature above 16ºC (61º F) and enough light, the quail would normally lay around 280 – 290 eggs a year. If you want to keep quails for their eggs, the best practice is to have a 3 to 1 hen to rooster rate, that’s when quail will lay the most eggs and it’s also an optimal rate if you want to breed them. The domesticated quail doesn’t make a nest and will not become a sitting hen so you would have to incubate the eggs for hatching. The Quail will start laying eggs at around 10-12 weeks of its age and will lay eggs actively for about 14-15 months if kept under optimal conditions. Apart from human consumption game bird keepers often feed their birds with boiled quail eggs and get brilliant results because of the high vitamin and nutrition volume.

If you would like to know more about the Japanese Quail or you're planning to keep quail please choose a topic from the main menu to learn more about these wonderful birds.

Golden Manchurian (Italian) QuailTexas Quail in grassland

Tuesday, January 20, 2015

YAJUE MAGONJWA MUHIMU YA KUKU/NDEGE WAFUGWAO ILI KUIKINGA NA KUIOKOA MIFUGO YAKO. [KUKU].


Ugonjwa ni nini? Ugonjwa ni mabadiliko kutoka katika afya ya kawaida ya mnyama/kuku. Hali hii hutokea pale
vimelea au vijidudu vinapoingia mwili wa mnyama, kwa kula vyakula vyenye sumu, au inapotokea kuna uhaba wa lishe au madini mwilini.
 
TOFAUTI ZA MUONEKANO KATI YA KUKU MWENYE AFYA NA KUKU MGONJWA
KUKU MWENYE AFYA NZURI
Ø  Macho na sura angavu
Ø  Hupenda kula na kunywa maji
Ø  Pua zilizo safi, upanga na undu mwekundu, manyoya
laini na yaliyopangika vizuri
Ø  Hupumua kwa utulivu
Ø  Sehemu ya kutolea haja huwa kavu
Ø  Kinyesi kikavu, cheupe na kisicho na rangi
Ø  Hutaga mayai kawaida
KUKU ASIYE NA AFYA NZURI
Ø  Huonekana mchovu na dhaifu
Ø  Hula na kunywa kidogo au zaidi ya kawaida
Ø  Hutoa kamasi puani, ute na matongotongo; manyoya
yaliyovurugika
Ø  Hupumua kwa shida na kwa sauti
Ø  Sehemu ya kutolea haja inakuwa na unyevunyevu na
kinyesi kuganda
Ø  Huharisha, kinyesi huwa na damu au minyoo
Ø  Hutaga mayai machache au husimama kutaga kabisa
Ø  Huwa na tabia ya kujitenga na wenzake katika kundi
MGONJWA MUHIMU YANAYOSABABISHWA NA BACTERIA
HOMA KALI YA MATUMBO (FOWL TYPHOID)
Maelezo: Ni ugonjwa wa kuku unaosababishwa na bacteria na hushambulia zaidi kuku
Wakubwa pia na vifaranga. Ugonjwa pia hushambulia aina zote za bata, kanga na ndege
wa porini.
Jinsi Ugonjwa Unavyoenea: Chanzo cha maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa
na kinyesi cha kuku wagonjwa. Panya, ndege na wanyama wengine wanaweza kueneza
ugonjwa kwa kubeba mizoga ya kuku waliokufa kwa ugonjwa na kuchafua maji na vyakula.
Maambukizi pia yanaweza kupitia katika mayai yanayototolewa na vifaranga kuathirika. Pia mashine za kutotolea zilizochafuliwa zinaweza kuambukiza vifaranga.


Dalili
Kuku wakubwa
Ø  Kuharisha kinyesi cha majimaji na cha rangi ya njano
Ø  Vifo vya ghafla
Ø  Kupauka kwa upanga na masikio kwa sababu ya kupungukiwa damu
Ø  Manyoya hutimka, hushusha mbawa, hufumba macho na kuzubaa (kuvaa koti)
Vifaranga
Ø  Vifaranga wanatotolewa wakiwa wamekufa au dhaifu
Ø  Hujikusanya pamoja na kukosa hamu ya kula
Ø  Kinyesi cha rangi ya njano na huganda kwenye manyoya ya sehemu ya kutolea haja
Ø  Hupumua kwa haraka na kwa shida
Ø  Vifo vingi huweza kutokea kuku wasipotibiwa
Uchunguzi wa Mzoga
Ø  Kinyesi cha rangi ya njano na kijani kwenye manyoya ya sehemu ya kutolea haja kubwa
Ø  Misuli iliyovia na damu kuwa nyeusi
Ø  Ini lililovimba na kuwa na rangi ya pinki
Ø  Bandama lililovimba
Ø  Figo na mayai yaliyovia
Ø  Mabaka meupe kwenye sehemu ya juu ya figo
Tiba
v  Yapo madawa mengi aina ya antibiotiki ambayo yanaweza kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa.
Lakini madawa haya hayawezi kumaliza kabisa ugonjwa kutoka shambani.
v  Pata ushauri wa daktari.

ZIFAHAMU TARATIBU NA RATIBA ZA UCHANJAJI WA KUKU KUANZIA VIFARANGA NA KUKU WAKUBWA.


TARATIBU NA RATIBA ZA UCHANJAJI
    Wakati wa kutayarisha mpango wa kuchanja kuku kwa ajili ya kinga dhidi ya magonjwa, kuna vipengele vikuu sita Ambavyo unatakiwa uvifahamu na kuvizingatia. Vipengele hivyo ni kama ifuatavyo:
1. Vifaranga vinavyoanguliwa kwa pamoja:
 Iwapo una kundi zaidi ya moja la vifaranga wanaoanguliwa,
Weka utaratibu wa chanjo ambao utapunguza uwezekano wa magonjwa kuenea shambani. Hivyo basi,
Hakikisha vifaranga na kuku wote wanapata chanjo kwa pamoja.
2. Umri wa kuchanja kuku:
Kwa kuku ambao wanatarajiwa kutaga mayai au kuwa kuku wazazi, chanjo
nyingi hutolewa si zaidi ya mwezi mmoja kabla ya kuku kuanza kutaga. Pia kuna baadhi ya chanjo ambazo haziruhusiwi kwa kuku wadogo. (Angalia Ratiba).
3. Magonjwa muhimu katika eneo husika:
Ni muhimu sana kuelewa magonjwa ya kuku yaliyopo katika eneo lako kabla ya kuandaa programu ya uchanjaji, hasa kwa yale magonjwa ambayo chanjo zenye
Vimelea hai hutumika. Hivyo basi, sio busara kuanza kutumia chanjo za aina hii katika maeneo ambayo
Ugonjwa huo haujawahi kuripotiwa.
4. Hali ya kiafya ya kuku watakaochanjwa:
 Usiwape chanjo kuku ambao wanaonyesha dalili za kuathirika kwa mfumo wa hewa au wanaonyesha kuwa na minyoo au wadudu wengine. Kwa kuku walio na dalili hizi chanjo zinaweza kuleta madhara na zisifanye kazi.
5. Aina ya kuku watakaochanjwa:
Kuku wanaofugwa kwa ajili ya nyama wanahitaji kinga ya muda mfupi, hivyo basi chanjo moja inaweza kutosha kabla ya kufikia umri wa kuuzwa. Lakini kuku wa mayai na kuku wazazi wanahitaji programu ya chanjo ambayo itawakinga na magonjwa kwa kipindi chote wanapokua na kutaga. (Zingatia Ratiba).
6. Historia ya Magonjwa katika shamba:
Kabla ya kuandaa mpango wa chanjo, lazima ufahamu ni
Magonjwa gani yaliyoenea katika shamba.
a) Kama unataka kuingiza kuku wapya kutoka mahali ambako ugonjwa umeshawahi kutokea,
kuku hao wachanjwe wiki 3 kabla ya kuwaingiza shambani
b) Iwapo utatumia chanjo yenye vimelea hai, hakikisha kwamba magonjwa hayo yameshawahi
kutokea katika shamba husika. Usitumie chanjo hizi katika shamba ambalo ugonjwa huo
haujawahi kutokea au kutambuliwa.
c) Wasiliana na mashamba jirani kufahamu iwapo wanatumia chanjo zenye vimelea hai. Toa taarifa
kwa mamlaka za mifugo iwapo unapanga kutumia chanjo hizo katika eneo lako. Pata ushauri wa daktari.

TARATIBU ZA UCHANJAJI
Mambo muhimu ya kuzingatia:                                                                                         
  •Hakikisha unazingatia kwa makini masharti ya mtengenezaji wa chanjo: jinsi ya kuhifadhi, kutayarisha na njia inayotumika kumchanja kuku. Wakati wote zingatia masharti ya mtengenezaji kuhusu uhifadhi wa chanjo ili isipoteze nguvu.     

Thursday, January 15, 2015

Ni rahisi sana kutunza kuku wa kienyeji: jifunze namna ya kuwatunza kuku wa kienyeji.


Unaweza kutunza kuku wa kienyeji na ukawa na kipato cha uhakika, pamoja na lishe nzuri kwa ajili ya familia.


Ulishaji: Kuku wa kienyeji wanaweza kulishwa kwa kumia mahindi, mchele, na mabaki ya ugali. Vyakula hivi ni lazima vikaushwe vizuri na kusagwa vizuri. Ulishaji ni lazima ufanyike katika sehemu safi au kwa kutumia vyombo vilivyotengenezwa maalumu kwa ajilii ya kulishia kuku.


Banda: Kuku wawe wa kienyeji au wa kisasa, wanahitaji kuwa na banda zuri kwa ajili ya malazi na kuwalinda. Wanahitaji chumba chenye nafasi ya kutosha na kinachopitisha hewa ya kutosha. Ni lazima kuwawekea fito kwa kuwa ndege hupenda kupumzika juu ya fito. Ni lazima banda la kuku lifungwe vizuri nyakati za usiku ili kuzuia wanyama wanaoweza kuwadhuru kuku. Ni lazima liwe safi wakati wote ili kuzuia magonjwa kama vile mdondo na mengineyo. Usitumie pumba za mbao au nguo kuukuu kwenye viota vya kutagia kwani huchochea kuwepo utitiri na funza wa kuku. Inashauriwa kutumia mchanga laini.


Maji ya kunywa: Kuku wapatiwe maji safi. Ni lazima kuangalia mara kwa mara na kuyabadilisha maji. Kamwe usiwape kuku maji machafu.


Chanjo: Chanjo kwa mifugo ni lazima ili kuzuia mashambulizi ya magonjwa. Magonjwa yaliyozoeleka ni kama vile Mdondo, Kideri, Ndui ya kuku, na homa ya matumbo (typhoid). Chanjo kwa kawaida hutolewa mara moja kwa kila baada ya miezi miwili.


Uwekaji wa kumbukumbu: Kumbukumbu zijumuishe aina ya ulishaji, namba ya uzalishaji, muda wa mwisho wa matumizi, kiasi cha malisho kwa kila siku, idadi ya vifo, na idadi ya mayai yaliyozalishwa.


Mwanzoni unahitaji nini?


Wafugaji walio wengi wanauliza wanahitaji nini katika hatua za awali ili kuweza kuanzisha mradi wa ufugaji wa kuku. Hii itategemea aina ya kuku uliochagua kufuga.


Ni busara kuwa na vifaa muhimu vinavyohitajika na viwe katika hali ya usafi kabla ya kuweka kuku bandani mwako. Kama unaanza na vifaranga, vifuatavyo ni vifaa muhimu vinavyohitajika kwa ajili ya vifaranga 200.


• Tenga na utengeneze banda zuri lenye joto na hewa ya kutosha wakati wote.
• Vyombo vinne (4) vya kunyweshea maji, hii ni katika wiki 2 za mwanzo na uongeze vyombo taratibu kulingana na kuku wanavyokua.
• Vyombo vinne (4) vya kulishia chakula, na viongezeke kulingana na kuku wanavyokua.
• Matandazo makavu na safi, inaweza kuwa maranda au mabua ya ngano.
• Pakiti moja au mbili za dawa ya Coccid (hii inapatikana katika maduka yote ya kilimo). Hata hivyo, utaratibu wa chanjo ni lazima ukamilishwe.
• Chakula kwa ajili ya vifaranga ambacho kimezalishwa na watengenezaji wanaoaminika.


Ufugaji wa kuku unaweza kuongeza kipato cha familia


“Mimi ni mfugaji mdogo wa kuku wa kienyeji katika viunga vya jiji la Dar es Salaam. Nina kuku 65 ambao ninawafuga katika eneo dogo nyumbani. Nilivutiwa kuanza ufugaji wa kuku wa kienyeji baada ya kutumia fedha nyingi kununua mayai ya kuku wa kienyeji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.